Gobani

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Gobani (alifariki Ufaransa, 670) alikuwa mmonaki padri wa Ukristo wa Kiselti kutoka Ireland.

Kama alivyothibitisha Beda Mheshimiwa[1], alikuwa mwanafunzi wa Fursei abati, aliyefanya kazi kubwa kueneza imani na umonaki kotekote katika visiwa vya Britania, hasa kati ya Waanglia[2][3].

Huyo alipohamia Ufaransa, Gobani alimfuata; hatimaye akawa mkaapweke kwenye msitu wa Voas, karibu na kijiji chenye jina lake, Saint-Gobain, Aisne.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, pengine mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 20 Juni[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads