Gregori Palamas
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Gregori Palamas (kwa Kigiriki Γρηγόριος Παλαμάς) (Konstantinopoli, 1296 – Thesalonike 1359) alikuwa mmonaki kwenye Mlima Athos (leo nchini Ugiriki) akawa Askofu mkuu wa Thesalonike na mwanateolojia maarufu hasa kwa kutetea Hesukia dhidi ya Barlaam wa Seminara.
Baadhi ya maandishi yake yamekusanywa katika Filokalia.
Anaheshimiwa kama mtakatifu katika Makanisa ya Kiorthodoksi, lakini pia katika baadhi ya Makanisa Katoliki ya Mashariki yanayofuata liturujia ya Ugiriki[1]
Makanisa hayo yanamheshimu hasa katika Dominika ya pili ya Kwaresima kuu (Dominika ya Gregori Palamas) pamoja na kumwadhimisha katika sikukuu yake tarehe 14 Novemba.
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Maandishi yake yanapopatikana
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads