Hudihudi

Ndege wa familia Upupidae wenye ushungi mrefu From Wikipedia, the free encyclopedia

Hudihudi
Remove ads

Hudihudi au ndututu ni ndege wa familia Upupidae wenye ushungi mrefu na domo refu na jembamba. Hudihudi wa Afrika huitwa jogoo-mwitu au kwembe kisunzu pia. Mwili una rangi ya machungwa lakini mabawa ni meusi yenye miraba myeupe na mkia pia ni mweusi na una mraba mweupe mmoja. Ndege hawa wanatokea maeneo wazi wa Afrika, Asia na Ulaya. Hutafuta chakula chini wakipenya ardhi kwa domo lao, pengine hukamata wadudu hewani. Hula wadudu hasa lakini watambaachi na vyura wadogo, mbegu na beri pia. Tago lao ni tundu mtini, katika ukuta wa nje au mwamba au ndani ya kando ya mchanga. Jike huyataga mayai 6-10.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads