Imhotep
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Remove ads
Imhotep (pia Immutef, Im-hotep au Ii-em-Hotep; aliitwa Imuthes (Ἰμούθης) na Wagiriki wa Kale; kwa hieroglifi ỉỉ-m-ḥtp "anayekuja kwa amani"; takriban karne ya 27 KK (~ 2650–2600 KK)) alikuwa mwandishi na mtaalamu wa Misri ya Kale.
Chini ya Farao Djoser wa nasaba ya tatu ya Misri Imhotep alikuwa afisa mtendaji mkuu. Anajulikana kama mhusika katika ujenzi wa piramidi ya Djoser.
Mara nyingi anatajwa kama msanifu wa kwanza anayejulikana[1] na pia mhandisi,[2] na tabibu katika historia anayejulikana kwa jina[3].
Hali halisi hatuna habari kamili juu yake isipokuwa maandishi ya kumsifu yaliyowekwa baada ya kifo chake. Hapo aitajwa kuwa "Mtendaji mkuu wa Farao, tabibu, mwakilishi wa kwanza wa mfalme wa Misri ya Juu, afisa mtawala wa Ikulu Kubwa, Kuhani Mkuu wa Heliopolis, Mjenzi Mkuu, Seremala Mkuu, Mchongaji Mkuu, Mfinyanzi Mkuu"[4]
Baada ya kifo chake aliheshimiwa kama mungu katika hekalu ya Memphis, baadaye pia kama mshairi na mwanafalsafa. Maneno yake yalinukuliwa mara nyingi [5].
Kaburi lake lilifichwa vema haikujulikana hadi leo hii [6] lakini wengi wanadhani iko mahali fulani huko Saqqara.

Remove ads
Marejeo
Kujisomea
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads