Isha Ramadhani

From Wikipedia, the free encyclopedia

Isha Ramadhani
Remove ads

Isha Ramadhani (amezaliwa 3 Februari 1982) ni mwimbaji na mtunzi mahiri wa nyimbo za taarab kutoka nchini Tanzania.

Ukweli wa haraka Maelezo ya awali, Jina la kuzaliwa ...
Remove ads

Anafahamika sana kwa kuwa mmoja kati ya walioanzisha kundi zima la taarab la Jahazi Modern Taarab. Kundi ambalo linaongozwa na Mzee Yusuf. Bi. Isha alizaliwa mkoani Mwanza, akiwa mtoto wa kwanza kati ya watoto watano katika familia yake. Alisoma shule ya msingi Mnazi Mmoja huko jijini Dar es Salaam kuanzia mwaka wa 1990 hadi 1996 alipomaliza darasa la saba.

Kwa bahari nzuri, kabahatika kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari, lakini aliishia kidato cha pili shuleni hapo kwa kutokana na matatizo mbalimbali ya kifamilia. Isha, ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Mara, hivi sasa ameolewa na ana watoto wawili. Anaishi na familia yake maeneo ya Tandale, Dar es Salaam.

Remove ads

Muziki

Mara yake ya kwanza kupanda jukwaani na kuimba na kundi la Jahazi, ilikuwa kwenye onyesho lililofanyika kwenye ukumbi wa bwalo la maofisa wa polisi, Oysterbay, Dar es Salaam. Katika onyesho hilo, aliimba wimbo wa "Hayanifiki" ambao umempatia umaarufu kwa kiasi kikubwa na kumfanya atambulike kwenye ulimwengu wa muziki wa taarab nchini Tanzania. Tangu hapo, akawa anashiriki kwenye vibao kadha wa kadha. Kibao hicho kilitungwa na Mzee Yusuf.

Miaka miwili baadaye, alifanikiwa kutunga wimbo wake mwenyewe, unaotambulika kwa jina la "Ya Wenzenu Midomo Juu". Wimbo ambao unapatikana kwenye albamu ya "VIP", ambayo ni ya nne kwa Jahazi. Wimbo huo ulimfanya awe juu na kuweza kupata mashabiki wengi zaidi kwenye ulimwengu wa mipasho.[1]

Remove ads

Maisha binafsi

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads