Julie Manning
Mwanasheria, Hakimu na mwanasiasa kutoka Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Julie Manning (alizaliwa Morogoro, 24 Januari 1939) alikuwa mwanasheria, na mwanasiasa wa Tanzania. Alikuwa mwanamke wa kwanza kusoma sheria nchini Tanzania, akawa Jaji wa Mahakama Kuu na Jaji Mkuu kabla ya kutumikia kama Waziri wa Sheria kutoka mwaka 1975 mpaka 1983.
Remove ads
Maisha
Katika mwaka 1963 Julie Manning alikuwa mwanamke wa kwanza kusoma sheria katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki. Baadae alisoma Sheria na kuwa "Law draughtswoman" katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.[1]
Mwaka 1973 alichaguliwa kuwa Hakimu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, alifanywa mwanamke wa kwanza kuwa Hakimu wa Mahakama kuu katika Afrika Mashariki na kati.[2] Mwaka 1975 alichaguliwa kuwa Waziri wa Sheria, kumfanya awe mmoja wa wanawake wawili wa kwanza kutumikia Baraza la mawaziri Tanzania.[3]
Jaji Joseph Warioba alikuwa Waziri wa Sheria mwaka 1983 baada ya Bi. Manning kutolewa katika wizara hiyo na kuwa mshauri katika Ubalozi wa Tanzania huko Washington.[4]
Remove ads
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads