Kapernaumu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kapernaumu
Remove ads

Kapernaumu (pia Kafarnaumu, kwa Kiebrania [1]כְּפַר נַחוּם, Kfar Nahum, yaani "Kijiji cha Nahum") ilikuwa kijiji cha uvuvi upande wa kaskazini wa Ziwa Galilaya kilichoanzishwa wakati wa ufalme wa ukoo wa Wahasmonei (karne ya 2 KK).[2]

Thumb
Sinagogi la Kapernaumu la karne ya 4 BK.
Thumb
Mabaki ya sinagogi (nguzo na mabenchi).
Thumb
Shinikizo la zeituni la wakati wa Roma ya Kale.
Thumb
Mabaki ya kijiji wakati wa Warumi.
Thumb
Misingi ya kanisa la karne ya 5 inayoonekana kupitia kioo.

Kilikuwa na wakazi 1,500 hivi[3] na masinagogi mawili. Nyumba iliyogeuzwa kuwa kanisa inasemekana ilikuwa ya Mtume Petro.

Kijiji kiliachwa mahame katika karne ya 11 BK.[4] This includes the re-establishment of the village during the Early Islamic period soon after the 749 earthquake.[4]

Remove ads

Katika Injili

Thumb
Mchoro wa James Tissot - "Uponyaji wa wakoma huko Kapernaumu" (Guérison des lépreux à Capernaum) - Brooklyn Museum.

Kapernaumu inatajwa na Injili zote nne (Math 4:13, 8:5, 11:23, 17:24, Mk 1:21, 2:1, 9:33, Lk 4:23, 31,7:1, 10:15, Yoh 2:12, 4:46, 6:17, 24,59). Inaonekana ilikuwa makao makuu (Math 4:12–17) ya kundi la Yesu lililozungukazunguka hasa katika mkoa wa Galilaya.

Huko Yesu alitoa mafundisho mengi na kufanya miujiza mingi; lakini kwa kutotubu ilipokea hukumu yake (Math 11:23).

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads