Kentauro
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kentauro (pia kantori, kantarusi) ni kiumbe cha hadithi za mitholojia ya Ugiriki ya Kale ambacho ni nusu farasi na nusu binadamu.


Jina
Jina lina asili katika Kigiriki κένταυρος kentauros, ila limekuwa centaurus kwa Kilatini na centaur kwa Kiingereza. Jina hilo liliingia katika Kiswahili kupitia Kiarabu قنطور qantur au قنطورس qantawrus. [1]
Mitholojia
Kuna hadithi mbalimbali katika mitholojia ya Kigiriki kuhusu asili ya viumbe hao. Mojawapo ni kwamba walitokea baada ya kubakwa kwa pepo ya mawingu ya kike[2]. Nyingine ilisimulia jinsi gani mwanaume alizaa kentauro na farasi.
Wanahistoria wanahisi kwmaba asili ya hadithi hizo ilikuwa mshtuko wa watu ambao hawakutumia farasi walipokutana mara ya kwanza na wageni waliopanda farasi ilhali walishindwa kutofautisha mnyama na binadamu.[3]
Kentauro walitazamwa mara kama wapiganaji wakali, mara kama viumbe wenye hekima kubwa.
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads