Kentauro

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kentauro
Remove ads

Kentauro (pia kantori, kantarusi) ni kiumbe cha hadithi za mitholojia ya Ugiriki ya Kale ambacho ni nusu farasi na nusu binadamu.

Thumb
Picha ya kuchongwa ya mapambano kati ya kentauro na binadamu (kutoka hekalu ya Parthenoni, Athini)
Thumb
Kentauro anayepambana na wanyama witu (mozaiki katika Villa Hadriana karibu na Roma, iliumbwa mnamo mwaka 130 BK)

Jina

Jina lina asili katika Kigiriki κένταυρος kentauros, ila limekuwa centaurus kwa Kilatini na centaur kwa Kiingereza. Jina hilo liliingia katika Kiswahili kupitia Kiarabu قنطور qantur au قنطورس qantawrus. [1]

Mitholojia

Kuna hadithi mbalimbali katika mitholojia ya Kigiriki kuhusu asili ya viumbe hao. Mojawapo ni kwamba walitokea baada ya kubakwa kwa pepo ya mawingu ya kike[2]. Nyingine ilisimulia jinsi gani mwanaume alizaa kentauro na farasi.

Wanahistoria wanahisi kwmaba asili ya hadithi hizo ilikuwa mshtuko wa watu ambao hawakutumia farasi walipokutana mara ya kwanza na wageni waliopanda farasi ilhali walishindwa kutofautisha mnyama na binadamu.[3]

Kentauro walitazamwa mara kama wapiganaji wakali, mara kama viumbe wenye hekima kubwa.

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads