Kikorsika

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kikorsika
Remove ads

Kikorsika (Corsu au lingua corsa) ni mojawapo ya lugha za Kirumi inayotumika na watu wasiopungua 150,000, hasa katika visiwa vya bahari ya Tireni. Inafanana sana na Kiitalia, hasa lahaja ya mkoa wake wa Toscana[1], kiasi kwamba wengine wanakiona Kikorsika kuwa lahaja, si lugha ya pekee.

Thumb
Kikorsika kinapotumika.
Thumb
Lahaja za Kikorsika.
Thumb
Mahusiano ya lugha za Kirumi.

Jina linatokana na kisiwa cha Korsika ambapo ilikuwa lugha ya kawaida hadi karne ya 20, ilipozidiwa na Kifaransa kiasi kwamba inaelekea kufa[2]. Kumbe inaendelea vizuri zaidi kaskazini mwa kisiwa jirani, Sardegna (Italia).

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads