Kolumba
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kolumba (anajulikana pia kama Colum Cille, Colm Cille, Calum Cille, Colum Keeilley, Kolban na Kolbjørn, maana yake "Njiwa wa Kanisa"; 7 Desemba 521 – 9 Juni 597) alikuwa mmonaki padri mmisionari kutoka Ireland aliyeeneza Ukristo kati ya Wapikti wa Uskoti.

Baada ya kupata malezi ya kitawa, alianzisha monasteri kadhaa maarufu kwa nidhamu na elimu, kwanza kwao, halafu katika kisiwa cha Iona (Uskoti) alipofariki mbele ya altare akiwa anamngojea Bwana[1].
Anahesabiwa kati ya Mitume kumi na wawili wa Ireland.
Remove ads
Sala yake
Peke yangu, pasipo yeyote ila wewe, Mungu wangu, nasafiri katika njia yangu.
Niogope nini, ukiwa karibu nami, mtawala usiku na mchana?
Katika mkono wako niko salama kuliko kama ningezungukwa na jeshi la kunilinda.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Marejeo ya lugha nyingine
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads