La Verna

From Wikipedia, the free encyclopedia

La Vernamap
Remove ads

La Verna, kwa Kilatini Alverna na kijiografia Monte Penna, ni mlima unaosimama peke yake hadi mita 1,283 katikati ya Apenini ya Toscana, juu ya bonde la Casentino, Italia ya Kati.

Thumb
Basilika la patakatifu pa La Verna.

Ni maarufu hasa kwa sababu inasemekana Fransisko wa Asizi, akiwa kwenye mfungo mkali juu yake miezi ya Agosti na Septemba 1224, alipata njozi ya Yesu msulubiwa aliyemtia mwilini madonda yake matano.

Baadaye palijengwa patakatifu panapovutia watu wengi. Mnamo Agosti 1921 Papa Benedikto XV alipatangaza basilika dogo.[1]

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads