Kidudu-deraya

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kidudu-deraya
Remove ads
Remove ads

Vidudu-deraya ni wanyama wadogo sana wa bahari wa oda Nanaloricida, oda pekee ya faila Loricifera wanaofunikwa na mabamba kama deraya. Wana urefu wa mm 0.1-1. Huishi katika masimbi ya sakafu ya bahari kwa vina vyote, aina zote za masimbi na latitudo zote[1].

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Wanyama hao wamefunua hivi karibuni kiasi. Faila yao imeelezewa mwaka 1983 na Kristensen. Mnamo 2021 spishi 43 zilikuwa zimeelezewa[2], lakini spishi nyingine 100 zinasalia kuelezewa[3].

Wana kiwiliwili kikubwa kilichozungukwa na mabamba sita ya deraya. Kichwa, ambacho hubeba miiba mingi iliyopinidika nyuma, huunganishwa na kiwiliwili kupitia shingo yenye pingili ambayo inaweza kurudishwa ndani ya deraya. Mdomo unaoweza kubenuliwa uko ncha ya mbele na umezungukwa na sindano nane. Ubongo umesitawi vizuri na umeunganishwa moja kwa moja na kila mwiba. Kamba ya neva hupita upande wa chini kuelekea ncha ya nyuma. Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula huanza na mfereji wa mdomo ambao unaweza kutolewa. Kisha hufuata koromeo ya umbo la tufe iliyo na misuli yenye nguvu na hatimaye utumbo ulionyooka ambao hufunguka katika mkundu mwishoni kabisa [4].

Remove ads

Picha

Marejeo

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads