Akili ya binadamu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Akili ya binadamu
Remove ads

Akili ya binadamu (kwa Kiingereza "mind"[3]) ni kipawa kinachowezesha kufikiri, kuelewa, kuwasiliana, kujifunza, kupanga na kutatua matatizo. Ni ufahamu unaotumia ubongo na unaomwezesha binadamu hata kutofautisha jambo kwa wema na ubaya wake upande wa maadili na hatimaye kumuongoza katika kufanya maamuzi kwa kutumia hiari yake[4].

Thumb
Ramani ya ubongo[1] ikionyesha sehemu zake zinavyohusika na kazi tofautitofauti.
Thumb
Mchoro wa René Descartes[2].

Dhana kuhusu asili ya akili ya binadamu zinatofautiana, vilevile na maelezo mengine mengi, kulingana na dini, falsafa na sayansi[5] husika.

Jambo mojawapo la msingi ni kuelewa kama akili hiyo ya pekee inategemea tu ubongo uliokua sana katika binadamu kuliko katika spishi nyingine au kuna athari kubwa ya roho ndani yake. Hii ni kwa sababu walichoweza kufanya watu hakifanani kabisa na wanyama walichofanya, hata wale walio na ujirani naye kibiolojia kama sokwe.

Remove ads

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads