Mkoa wa Kayes
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mkoa wa Kayes (kwa Kibambara: Kayi Dineja) ni mojawapo ya mikoa nane nchini Mali inayoitwa regions. Eneo lake ni kilomita za mraba 120,760. Idadi ya wakazi ilikuwa takriban milioni 2 kwenye mwaka 2009. Makao makuu yako mjini Kayes . Mkoa huo kihistoria ulikuwa sehemu ya Dola la Ghana na Milki ya Mali.


Remove ads
Jiografia
Mkoa wa Kayes umepakana na Mauritania upande wa kaskazini, Senegal upande wa magharibi, Guinea upande wa kusini na upande wa mashariki uko Mkoa wa Koulikoro .
Makabila ya eneo hilo ni pamoja na Wasoninke, Wakhassonke, Wamalinke, Wadialonke na Wafulani.
Mito ya mkoa ni pamoja na Baoule, Bafing na Bakoy ambayo inaungana katika mji wa Bafoulabe kuunda Mto Senegal.
Miji mikubwa katika eneo ni Kayes, Kita, Bafoulabé, Nioro du Sahel, Diéma, Yélimané, Sadiola na Kéniéba.
Remove ads
Wilaya
Mkoa wa Kayes umegawiwa katika wilaya 7 zinazoitwa cercles: [1]
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads