Mti wa uzima

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mti wa uzima
Remove ads

Mti wa uzima (kwa Kiebrania עֵץ הַֽחַיִּים, Etz haChayim,) ni mfano unaotumiwa na Biblia.[1]

Thumb
Anguko la mtu lilivyochorwa na Lucas Cranach katika karne ya 16, mti wa uzima ukiwepo upande wa kushoto karibu na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Katika kitabu cha Mwanzo, mti wa uzima unapatikana katika mstari 2:9 kama mti uliopandwa na YHWH Elohim (יְהוָה אֱלֹהִים) karibu na mti wa ujuzi wa mema na mabaya (עֵץ הַדַּעַת) "katikati ya bustani ya Eden".[2]

Katika 3:24 imeandikwa kwamba baada ya dhambi ya asili kerubi analinda njia inayofikia mti wa uzima.

Kitabu cha Mithali kinatumia jina hilo mara nne (3:18, 11:30, 13:12 na 15:4).

Hatimaye Kitabu cha Ufunuo kinatumia usemi wa Kigiriki ξύλον (τῆς) ζωής, xylon (tēs) zōës, mara nne vilevile (2:7, 22:2, 22:14 na 22:19.

Thumb
Milango ya kifalme iliyochongwa kudokeza mti wa uzima, Chotyniec, Polandi.

Kwa kawaida Wakristo wamechukua usemi huu kama wa fumbo kwa msalaba wa Yesu.

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads