Mwambatope
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mwambatope (kwa Kiingereza: shale rock) ni aina ya mwamba mashapo yenye chembe ndogo sana; asili yake ni mashapo ya matope.

Matope yanayofanya mwambatope ni ya udongo wa mfinyanzi (clay) pamoja na chembe ndogo za kwatzi na kalsiti.[1]

Mara nyingi mwambatope yanatokea kwa matabaka membamba yanayoweza kutenganishwa kirahisi. Kama aina hii ya mwambatope inaathiriwa na shinikizo na joto kubwa zaidi itakuwa mwamba metamofia aina ya grife unaovunjika kwa urahisi kwa bapa nyembamba kama sahani yaani sleti. Hizo zinatumiwa kama bapa za kuezeka mapaa ya nyumba.
Remove ads
Kutokea kwa mwambatope
Matope yatakayounda mwambatope hukusanyika katika maji yenye mwendo wa polepole au pale ambapo mito inaishia ziwani, katika delta ya mto au katika vilindi vya baharini pasipo mikondo ya bahari. Mchakato wa kukusanyika na kuwa mwamba unachukua mamilioni ya miaka.
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads