Ndege-mawingu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Ndege-mawingu ni ndege wa bahari katika jenasi Phaethon, jenasi pekee ya familia Phaethontidae. Ndege hawa ni weupe na wana mileli mirefu katikati ya mkia. Hupitisha maisha yao yote baharini isipokuwa wakati wa majira ya kuzaa. Wanaweza kuogelea na kwa hivyo wana ngozi kati ya vidole; kwa kweli hawatembei vizuri. Huwakamata samaki na ngisi wakipiga mbizi au huwakamata panzi-bahari (samaki wanaoruka juu ya maji). Jike hutaga yai moja tu ndani ya tundu au mwanya wa mwamba visiwani kwa bahari.
Remove ads
Spishi za Afrika
- Phaethon aethereus, Ndege-mawingu Domo-jekundu (Red-billed Tropicbird)
- Phaethon lepturus, Ndege-mawingu Mkia-mweupe (White-tailed Tropicbird)
- Phaethon rubricauda, Ndege-mawingu Mkia-mwekundu (Red-tailed Tropicbird)
Picha
- Ndege-mawingu domo-jekundu
- Ndege-mawingu mkia-mwekundu
- Ndege-mawingu mkia-mweupe
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads