Nikodemo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Nikodemo (kwa Kigiriki Νικόδημος, Nikodemos) alikuwa mwalimu wa Torati wa madhehebu ya Mafarisayo tena mwanabaraza wa Baraza la Israeli katika karne ya 1 BK.

Anaheshimiwa na Wakristo wengi kama mtakatifu, ingawa sikukuu yake inaadhimishwa katika tarehe tofautitofauti, hasa tarehe 31 Agosti[1].
Remove ads
Nikodemo katika Injili
Anajulikana kwa sababu ya kutajwa mara kadhaa katika Injili ya Yohane,[2] kama mtu aliyevutiwa na Yesu Kristo ingawa aliogopa maneno ya Wayahudi wenzake.
Ndiyo sababu alimtembelea usiku ili kumuuliza maswali ya dini yao bila kujulikana (Yoh 3:1–21).
Baadaye katika baraza alimtetea Yesu kwamba si haki kuhukumu mtu bila kumsikiliza kwanza, lakini alinyamazishwa (Yoh 7:50–51).
Hatimaye alimsaidia Yosefu wa Arimataya, ambaye alitarajia Ufalme wa Mungu uliotangazwa na Yesu, akachukua jukumu la kumzika (Yoh 19:39–42) [3].
Remove ads
Nikodemo katika picha
- Nicodemus (left) talking to Jesus, by Henry Ossawa Tanner
- Christus und Nicodemus, by Fritz von Uhde (1848–1911)
- Entombment, by Tizian
- Jesus and Nicodemus by Crijn Hendricksz, 1616–1645
- Cima da Conegliano, Nicodemus with Christ's body, Apostle John on the right and Mary to left.
- Entombment, by Pietro Perugino, with Nicodemus and Joseph from Arimatea
- Nicodemus (right) talking to Jesus, by William Brassey Hole, (1846–1917)
- Tanner - Nicodemus coming to Christ II
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads