Paulo Miki

From Wikipedia, the free encyclopedia

Paulo Miki
Remove ads

Paulo Miki (Kyoto, takriban 1565 Nagasaki, 5 Februari 1597) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki nchini Japani.

Thumb
Mtakatifu Paulo Miki

Ametambuliwa kuwa mtakatifu kama mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 6 Februari[1].

Maisha

Paulo Miki alizaliwa nchini Japani kati ya miaka 1564 na 1566.

Alijiunga na Shirika la Yesu (Wajesuiti), akahubiri Injili kwa ufanisi [2].

Lakini dhuluma dhidi ya Wakatoliki zilipozidi, yeye na wenzake 25 (mapadri na watawa 8 na walei 17[3]) walikamatwa, walitukanwa na kuteswa vikali, na hatimaye wakasulubiwa huko Nagasaki tarehe 5 Februari mwaka 1597, huku wakifurahia neema ya kuuawa namna ileile ya Yesu [4].

Hadi sasa Wafiadini wa Japani waliotangazwa watakatifu ni 42, mbali na wenye heri 393.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads