Paulo wa Tebe

From Wikipedia, the free encyclopedia

Paulo wa Tebe
Remove ads

Paulo wa Tebe (230 hivi - Jangwa la Thebe, 5 Januari 342) anakumbukwa kama mkaapweke wa Kikristo wa kwanza nchini Misri.

Thumb
Picha ya Kikopti ya Paulo wa Tebe.
Thumb
Paulo wa Tebe, José de Ribera, 1640.
Thumb
Mt. Antoni abati na Mt. Paulo Mkaapweke walivyochorwa na Diego Velázquez, 1635 hivi - Museo del Prado, Madrid (Hispania).
Thumb
Mt. Antoni abati na Mt. Paulo Mkaapweke.

Anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi tangu zamani sana kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 10 Januari[1] au 15 Januari[2].

Remove ads

Maisha

Chanzo cha habari kuhusu maisha yake ni kitabu cha Jeromu, Vita Sanctii Pauli primi eremitae, kilichoandikwa katika nusu ya pili ya karne IV.

Wakati wa dhuluma ya Kaisari Decius, Paulo, kijana msomi na tajiri wa Misri, alilazimika kukimbia mji wake na kwenda jangwani kisha kushtakiwa na jamaa zake (waliotamani kujipatia mali yake) kuwa ni Mkristo.

Baada ya dhuluma hiyo kali kwisha mapema, Paulo hakurudi nyuma, bali aliendelea kuishi upwekeni hadi kifo chake.

Alipokaribia kufa alitembelewa na Antoni Abati, akamuomba amzike amefunikwa joho alilopewa na Atanasi wa Aleksandria.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo kwa Kiswahili

Vyanzo kwa lugha nyingine

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads