Kitororo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kitororo
Remove ads

Vitororo au kongogolo ni ndege wadogo wa jenasi Pogoniulus katika familia Lybiidae. Ndege hawa ni matoleo madogo ya zuwakulu na mwenendo wao ni takriban sawa na hawa. Vitororo ni ndege wadogo wenye 9-12 cm na 7-15 g. Wana rangi ya kijivu, nyeusi au majani, mistari myeupe na madoa mekundu au njano. Hula wadudu na beri, matini madogo na beri za spishi za kirukia hasa. Dume na jike pamoja huchimba tundu katika tawi au shina lililooza na jike huyataga mayai 2-4 ndani yake.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Remove ads

Spishi

Remove ads

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads