Reptilia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Reptilia
Remove ads
Remove ads

Reptilia (kutoka Kilatini "reptilis" mwenye kutambaa; pia: mtambaazi, mtambaachi, mnyama mtambaaji[1]) ni kundi la wanyama wenye damu baridi, ngozi ya magamba badala ya nywele au manyoya wakipumua kwa mapafu. Siku hizi wataalamu hupendelea jina Sauropsida.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Wanazaa kwa njia ya mayai; wengine wanataga mayai na wadogo wanatoka nje bila ngazi ya kiluwiluwi au kwa spishi kadhaa mayai yanaiva ndani ya tumbo la mama na wadogo wanazaliwa hai.

Kibiolojia ni ngeli ya vertebrata. Jina limetokana na maumbile yao maana wanatambaa na tumbo juu ya ardhi; ama kwa miguu mifupi kama mijusi au bila miguu kama nyoka.

Remove ads

Mwainisho

  • Ngeli Reptilia (au Kladi Sauropsida)
    • Kladi Eureptilia
      • Kladi Romeriida
        • Nusungeli Anapsida
        • Nusungeli Diapsida
          • Ngeli ya chini Archosauromorpha

              • Oda Saurischia
                • Nusuoda Theropoda
            • Oda ya juu Crocodylomorpha
          • Ngeli ya chini Lepidosauromorpha
            • Oda ya juu Lepidosauria

Dinosauria wa kale walikuwa reptilia wakubwa sana walikwisha miaka milioni 65 iliyopita. Kufuatana na vumbuzi za hivi karibuni ndege hufikiriwa kuwa na nasaba na dinosauri (kutoka kwa nusuoda ya Theropoda).

Remove ads

Maelezo

Loading content...

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads