Retisi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Retisi (pia: Reticius, Rheticius, Rheticus, Rhétice; alifariki 320 hivi) kwa miaka 25 hivi alikuwa askofu wa Autun, leo nchini Ufaransa, akiwa wa kwanza kati ya wanaojulikana [1][2].

Kwa agizo la kaisari Konstantino Mkuu alishiriki sinodi mbili zilizojaribu kumaliza farakano la Donato lilitokea Afrika Kaskazini[3].

Gregori wa Tours alimsifu katika maandishi yake [3] na Jeromu alimtaja pamoja na vitabu viwili alivyoviandika[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Mei[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads