Rudolf Sherwin

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rudolf Sherwin
Remove ads

Rudolf Sherwin (Rodsley, Derbyshire, 25 Oktoba, 1550Tyburn, 1 Desemba 1581) alikuwa padri wa Uingereza maarufu kwa akili na imani[1].

Thumb
Bango mahali alipozaliwa.

Mwaka mmoja baada ya kupata digrii ya pili aliacha ushirika wa Anglikana ili kujiunga na Kanisa Katoliki, alipata upadrisho huko Ufaransa mwaka 1577, alikwenda Roma alikokaa miaka 3[2], halafu akatumwa kwao alipofanya utume kwa siri miezi michache tu[3].

Alipokuwa gerezani mwaka mzima aliongoa wengi na hatimaye alinyongwa na kukatwa vipandevipande. Maneno yake ya mwisho yalikuwa: "Iesu, Iesu, Iesu, esto mihi Iesus!"[4].

Alitangazwa mwenye heri na Papa Pius IX mwaka 1929 na mtakatifu mwaka 1976 na Papa Paulo VI.

Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki tarehe 1 Desemba[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads