Mlali (ndege)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mlali (ndege)
Remove ads

Mlali au sekini ni ndege wa jenasi Prionops, jenasi pekee ya familia Prionopidae. Wanatoka Afrika kusini kwa Sahara tu. Spishi za Asia ambazo ziliainishwa katika familia hii, zimehamishwa ndani ya familia Tephrodornithidae. Mlali ni weusi na weupe, weusi na rangi ya kijivu au weusi, weupe na rangi ya kijivu pengine pamoja na rangi ya kahawia nyekundu kwa tumbo. Domo lao lina ncha kwa kulabu na rangi ya nyeusi au nyekundu; miguu ni myekundu mara nyingi. Ndege hawa wana ngozi yenye rangi kali (nyekundu au pinki) kuzunguka macho na ushungi kwa umbo wa helmeti wenye rangi ya nyeupe, kijivu, nyeusi au manjano. Hula wadudu na vertebrata wadogo. Hulijenga tago lao kwa vipande vya gome na tandabui mtini au kichakani na jike hutaga mayai 2-5.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi

Remove ads

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads