Sengi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Sengi
Remove ads

Sengi, njule au isanje ni wanyama wadogo wa familia Macroscelididae. Jina la njule litumika kwa jenasi Rhynchocyon na isanje litumika kwa Petrodromus tetradactylus. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika maeneo mbalimbali. Sifa bainifu mno ya sengi ni pua yao refu sana ambayo wanaweza kuipota ili kutafuta chakula. Hii inafanana kidogo na mwiro wa tembo na ni chimbuko cha jina lao la Kiingereza "elephant shrew". Miguu yao ni mirefu kwa kulinganisha na huenda wakirukaruka kama sungura. Rangi yao ni kahawia au kijivu kwa kawaida lakini spishi nyingine zina rangi kali pia kama nyekundu au njano. Hula invertebrata kama wadudu, buibui, majongoo, tandu na nyunguyungu.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi

Remove ads

Picha

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads