Servulo wa Roma

From Wikipedia, the free encyclopedia

Servulo wa Roma
Remove ads

Servulo wa Roma (alifariki Roma, Italia, 23 Desemba 590) alikuwa ombaomba jijini Roma aliyelala tangu utotoni mbele ya kanisa la Mt. Klementi kutokana na hali yake ya kupooza mwili mzima[1].

Thumb
Mt. Servulo alivyochorwa.

Pamoja na mateso yake hayo, aliishi kwa imani kubwa, akimshukuru Mungu na kuwagawia maskini wenzake alichopewa na wafadhili.

Papa Gregori I aliandika juu yake sura moja ya kitabu cha Majadiliano.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 23 Desemba[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads