Simoni wa Crepy

From Wikipedia, the free encyclopedia

Simoni wa Crepy
Remove ads

Simoni wa Crepy (au wa Vexin; Bar-sur-Aube, Ufaransa, 1048 hivi - Roma, Italia, 30 Septemba 1082) alikuwa mtawala wa Amiens, Vexin na Valois miaka 1074-1077.

Thumb
Sanamu yake.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 30 Septemba[1].

Maisha

Baada ya kuoa, alikubaliana na mke wake waachane na mali yao wakatawe monasterini. Hata hivyo, kwa kutoridhika na utajiri wa mazingira ya Condat, baadaye alikwenda kuishi upwekeni kwenye misitu ya Jura.

Kutoka huko aliitwa mara kadhaa kufanya upatanisho kati ya watawala waliopigana vita.

Pia alihiji hadi Nchi takatifu halafu Roma alipofariki huku akisaidiwa sakramenti za mwisho na Papa Gregori VII.

Alizikwa kwenye basilika la Mt. Petro[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads