Suzana U Surim

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Suzana U Surim (1803 - Seoul, 20 Septemba 1846) ni mmojawapo katika kundi kubwa la Wakristo wa Kanisa Katoliki nchini Korea waliouawa kwa ajili ya imani yao katika miaka 17911888. Wanakadiriwa kuwa 8,000 - 10,000.

Mjane huyo na wafiadini wenzake 102 walitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa watakatifu tarehe 6 Mei 1984.[1]

Sikukuu ya hao Wafiadini wa Korea huadhimishwa tarehe 20 Septemba[2].

Walionyongwa katika magereza mbalimbali siku moja naye ni: Laurenti Han Ihyong, Petro Nam Kyongmun, Yosefu Im Chipek, Teresa Kim Imi, Agata Yi Kannan na Katerina Chong Choryom[3].

Remove ads

Mazingira

Mwishoni mwa karne ya 18, Ukristo wa Kikatoliki ulianza kuenea taratibu katika rasi ya Korea, nchi ya Kikonfusyo, kwa juhudi na ari za wananchi walei[4].

Mwaka 1836 Korea ilipata wamisionari wa kwanza kutoka nje (wanashirika wa Paris Foreign Missions Society) ambao walilisha na kuthibitisha imani kwa kutangaza Neno la Mungu na kuadhimisha sakramenti.

Chini ya nasaba ya Joseon, Ukristo ulifutwa, tena waamini walidhulumiwa na kuuawa. Waliobaki walipaswa kushika imani yao kwa siri.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads