Taiga

From Wikipedia, the free encyclopedia

Taiga
Remove ads

Taiga (kwa Kiingereza[1] pia boreal forest [2] au snow forest [3]) ni jina la maeneo makubwa ya misitu kaskazini mwa dunia inayofanywa na aina mbalimbali ya miti ya misunobari, katika Eurasia pia pamoja na mibetula. Takriban 29% za misitu yote duniani ni aina ya taiga.

Thumb
Uenezaji wa taiga duniani, inapatikana katika kaskazini kama kanda pana kati ya taiga na mbuga baridi.
Thumb
Misonobari kwenye taiga ya Alaska.

Taiga inafunika sehemu kubwa za Alaska, Kanada, Uswidi, Ufini, Norwei, Kazakhstan ya kaskazini na Urusi (hasa Siberia) pamoja sehemu nyingine za kaskazini za Marekani.

Maeneo ya taiga yako upande wa kusini wa kanda la tundra. Katika Urusi taiga inafuatwa na kanda la mbuga baridi kusini mwake.

Kwa jumla tabianchi kwenye taiga ni baridi sana kwa miezi mingi ya mwaka[4]. Majirajoto ni fupi, kwa kawaida miezi 1-2 pekee. Taiga ya Siberia wastani ya halijoto wakati wa baridi ni kati ya -6°C na -50°C.[5]

Remove ads

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads