Ng'ombe (kundinyota)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Ng'ombe (pia Tauri, kwa Kilatini na Kiingereza Taurus) [1] ni jina la kundinyota kwenye nusutufe ya kaskazini ya dunia yetu.



Mahali pake
Ng'ombe iko angani kwenye mstari wa Zodiaki kati ya Kondoo (pia Hamali, lat. Aries) upande wa magharibi na Mapacha (pia Jauza, lat. Gemini) upande wa mashariki.
Inapaka na kundinyota jirani za Hudhi (Auriga), Farisi (Perseus), Hamali (Kondoo) (Aries), Ketusi (Cetus), Nahari (Eridanus), Jabari (Orion) na Jauza (Mapacha) (Gemini).
Ng'ombe - Taurus ni sehemu ya zodiaki maana yake mstari wa ekliptiki unapita humo. Ilhali miendo ya Mwezi na sayari inafuatana karibu na ekliptiki magimba haya huonekana katika eneo la Tauri kwa wakati fulani kwenye mwaka.
Remove ads
Jina
Ng'ombe ni tafsiri ya Tauri. Mabaharia Waswahili walijua nyota hili tangu miaka mingi kwa jina Tauri. Walipokea jina hili kutoka Waarabu wanaosema ثور thawr ambalo linamaanisha fahali[2]. Waarabu walitafsiri hapa jina la Ptolemaio aliyetaja nyota hizi vile kwa jina la Ταῦρος tauros yaani fahali katika orodha yake ya Almagesti[3].
Wagiriki wa Kale waliwahi kupokea kundinyota hili likiangaliwa kama fahali kutoka utamaduni wa Babeli. Katika mitholojia ya Wagiriki kuna hadithi mbalimbali zilizosimuliwa hapa. Hasahasa waliona fahali kwenye anga kama ishara ya mungu mkuu Zeus aliyechukua umbo la fahali alipomtongoza binti Europa; Zeus alibadilisha umbo lake akaingia katika kundi la ng'ombe waliochungwa na Europa. Siku mmoja Europa alipanda juu ya fahali na hapo Zeus alikimbia naye hadi kisiwa cha Kreta; hapa alizaa naye wana watatu akamfanya Europa malkia wa kwanza wa Kreta. Aliweka umbo la fahali kati ya nyota kama kumbukumbu ya mapenzi yake.
Katika unajimu wa kisasa katika Afrika ya Mashariki jina "Tauri" limesahauliwa badala yake kundinyota hili linaitwa kwa tafsiri tu ya "Ng'ombe".
Ng'ombe - Taurus ni kati ya makundinyota 48 zilizotajwa tayari na Klaudio Ptolemaio katika kitabu cha Almagesti wakati wa karne ya 2 BK. Iko pia kati ya makundinyota 88 yanayoorodheshwa na Umoja wa kimataifa wa astronomia [4] kwa jina la Taurus. Kifupi chake rasmi kufuatana na Ukia ni 'Taui'.[5]
Remove ads
Nyota
Nyota za Ng'ombe huwa haziko pamoja kihalisi lakini zinaonekana tu vile kutoka duniani. Kwa uhalisi kuna umbali mkubwa kati yao, kama ziko mbali au jirani nasi. Kwa hiyo kundinyota "Ng'ombe" linaonyesha eneo la angani jinsi tunavyoliona kutoka Duniani.
Kuna nyota nyingi katika eneo la kundinyota hili na hasa Dabarani (en:Aldebaran), inaitwa pia Alfa Tauri, ambayo ni nyota jitu jekundu ikiwa kati ya nyota angavu zaidi zinazoonekana angani[6].
Kuna nebula la Messier 1 inayojulikana pia kwa jina la Nebula ya Kaa (en:crab nebula)[7]. Ni mabaki ya nyota nova ambayo mlipuko wake ulirekodiwa huko China mwaka 1054 baadaye pia Japani[8].
Fungunyota la Kilimia (en:Pleiades) linaonekana vema kwa macho matupu katika kaskazini ya Ng'ombe.[9], [10]
Tanbihi
Viungo vya Nje
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads