Akoliti

From Wikipedia, the free encyclopedia

Akoliti
Remove ads

Akoliti (kwa Kiingereza "acolyte", kutoka Kigiriki ἀκόλουθος, akoluthos, yaani "msindikizaji") ni Mkristo anayemsaidia askofu, padri au shemasi anapoongoza ibada fulani[1].

Thumb
Akoliti alivyochorwa na Abraham Solomon, 1842.
Thumb
Akoliti wa Armenia akishika "ripida".
Thumb
Akoliti wa Kanisa la Kilatini akimshikilia askofu kitabu cha ibada wakati wa kuweka wakfu altare.

Katika Kanisa la Kilatini

Katika Kanisa la Kilatini tangu mwaka 1972, pamoja na usomaji, ni mojawapo kati ya huduma mbili za lazima[2] ambazo wale wote wanaojiandaa kupata daraja takatifu wazipate na kuzitekeleza kwa muda fulani.

Kati ya kazi muhimu za akoliti, mojawapo ni kuwagawia waamini wenzake sakramenti ya ekaristi[3].

Kuanzia mwaka 2021 wanawake pia wanaweza kupewa kazi hiyo, baada ya Papa Fransisko kurekebisha kanuni 230 ya Mkusanyo wa Sheria za Kanisa.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads