Utamadunisho

From Wikipedia, the free encyclopedia

Utamadunisho
Remove ads

Utamadunisho (kwa Kiingereza "enculturation") ni mchakato wa mtu kupokea utamaduni wa wale wanaomzunguka[1] ili kuingia zaidi katika maisha ya jamii husika.

Thumb
Makundi ya watoto na vijana ndiyo njia mojawapo muhimu ya utamadunisho.

Katika Ukristo

Watoto wakicheza wakati wa Misa katika kanisa kuu la Basankusu, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katika Ukristo msamiati huo unamaanisha hasa mchakato wa ujumbe wa Injili kuingia kwa dhati zaidi katika maisha ya watu wa utamaduni fulani ili Kanisa lizidi kutia mizizi katika kabila au taifa husika badala ya kubaki kasumba.

Mchakato huo hauwezi kufanyika mara moja, bali unadai uwazi wa waumini kwa Neno la Mungu na kwa Roho Mtakatifu pamoja na jitihada za makusudi na za pamoja.

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads