Valentinus

From Wikipedia, the free encyclopedia

Valentinus
Remove ads

Valentinus (Terni, Italia, 176 hivi - Roma, 14 Februari 273) alikuwa askofu wa Terni.

Thumb
Mt. Valentinus akimbatiza Mt. Lusila, mchoro wa Jacopo Bassano.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini katika Kanisa Katoliki, lakini pia na Waorthodoksi, Waanglikana na Walutheri kadhaa.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Februari ya kila mwaka[1].

Valentinus anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na sikukuu yake kuadhimishwa kote duniani kama Valentine's Day.

Remove ads

Historia

Historia yake inawezekana inamchanganya na Valentinus mwingine, padri wa karne ya 3 huko Roma, aliyeuawa mwaka 269 katika mazingira yaleyale [2].

Hadithi

Kuna hadithi mbalimbali juu yake. Mojawapo inasema Valentinus aliandika barua kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani; mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya: Kutoka kwa Valentinus wako.

Mbali ya hadithi, askofu huyo alijulikana kwa miujiza yake. Huko Terni, mnamo 2011, ilipatikana mifupa ya Sabino e Serapia: mmoja alikuwa Mpagani akida wa jeshi la Roma, mwingine msichana Mkristo motomoto. Kwa ajili yake Sabino aliongokea Ukristo, lakini baada ya muda mfupi aligundua kwamba Serapia ni mgonjwa wa kifua kikuu. Ili asitengane naye, Sabino alimuomba Valentinus, naye alibariki ndoa yao na kuomba mapendo yao yadumu milele. Baadaye walifariki pamoja wamekumbatiana na ndivyo mifupa yao inavyopatikana hadi leo.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads