Warshawa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Warshawa (kwa Kipoland: Warszawa; kwa Kiingereza Warsaw) ni mji mkuu wa Poland pia mji mkubwa wa nchi, wenye wakazi milioni mbili hivi (1.78 mln - 2018).
Remove ads
Jiografia
Warshawa iko katikati ya bonde la mto Vistula (Kipoland: polnisch Wisła, takriban km 350 kutoka Bahari Baltiki.
Historia
Warshawa imekuwa mji tangu karne ya 13, ikawa mji mkuu wa Poland mwaka 1596.
Iliharibiwa mara nyingi katika historia yake, hasa wakati wa vita kuu ya pili ya dunia. Wapoland walijaribu kuasi dhidi ya Wajerumani walioshika mji kati ya miaka 1939 na 1944; pamoja na vifo vingi, asilimia 90 za nyumba zote ziliharibiwa.
Baada ya vita mji ulijengwa upya mara nyingi kwa kurudisha nyumba zinazofanana na nyumba za kale.
Kitovu chake kimeorodheshwa na UNESCO kati ya mahali pa Urithi wa Dunia.
Remove ads
Utamaduni
Kuna vyuo 66 pamoja na Chuo Kikuu cha Warshawa, vyuo vikuu vingine, nyumba za maigizo, opera na makumbusho mbalimbali.
Uchumi
Warshawa ni mji wa viwanda vingi vya kutengenezea chuma, mashine, motokaa na mengine mengi.
Picha za Warshawa
- Jumba la utamaduni na sayansi
- Kituo cha Metro ya Warshawa
- Jumba la kifalme
- Ikulu ya rais
- Mji wa Kale
- Belweder
- Jumba la Ujazdowski
- Kanisa la Aleksander
Tazama pia
Viungo vya nje
- Tovuti rasmi Ilihifadhiwa 16 Novemba 2007 kwenye Wayback Machine.
- Tovuti ya utalii wa Warshawa Ilihifadhiwa 12 Agosti 2005 kwenye Wayback Machine.
- Ramani Ilihifadhiwa 28 Januari 2011 kwenye Wayback Machine.
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Poland bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Warshawa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads