Yusto Ranfer
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Yusto Ranfer, M.E.P. (Chalon-sur-Saône, Saône-et-Loire, Ufaransa, 28 Februari 1838 - Sai-Nam-Hte, 7 Machi 1866) ni mmojawapo katika kundi kubwa la Wakristo wa Kanisa Katoliki nchini Korea waliouawa kwa ajili ya imani yao katika miaka 1791–1888. Wanakadiriwa kuwa 8,000 - 10,000.

Padri huyo mmisionari alikatwa kichwa pamoja na askofu Simeoni-Fransisko Berneux na mapadri wawili wa shirika lake: Alois Beaulieu na Petro-Henri Dorie kwa sababu, walipoulizwa na watesi wamefika Korea kufanya nini, walijibu kwa ujasiri na unyofu kwamba wana lengo la kuokoa watu kwa jina la Yesu[1].
Hao na wafiadini wenzao 99 walitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa watakatifu tarehe 6 Mei 1984.[2]
Sikukuu ya hao Wafiadini wa Korea huadhimishwa tarehe 20 Septemba.
Remove ads
Mazingira
Mwishoni mwa karne ya 18, Ukristo wa Kikatoliki ulianza kuenea taratibu nchini[3] kwa juhudi za wananchi walei. Mwaka 1836 Korea, nchi ya Kikonfusyo ilipata wamisionari wa kwanza kutoka nje (wanashirika wa Paris Foreign Missions Society)[4].
Chini ya nasaba ya Joseon, Ukristo ulifutwa, tena waamini walidhulumiwa na kuuawa. Waliobaki walipaswa kushika imani yao kwa siri.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Marejeo ya lugha nyingine
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads