Mzeituni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mzeituni au mzaituni (jina la kisayansi kwa Kilatini Olea europaea, yaani "mzeituni wa Ulaya", au Olea sylvestris, yaani "mzeituni mwitu") ni mti mfupi wa familia ya Oleaceae unaopatikana hasa kandokando ya Bahari ya Kati, lakini pia sehemu nyingine za Afrika na Asia.[1]
Matunda yake (zeituni au zaituni) ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa mafuta (90%), ingawa yanaliwa pia bila kushindiliwa (10%).
Inaonekana asili ya ulimaji wake ni Uajemi na Mesopotamia miaka 6,000-7,000 iliyopita. Kutoka huko ulienezwa sehemu nyingine.
Leo uzalishaji ni mkubwa hasa Hispania, halafu Italia, Ugiriki, Uturuki n.k.
Mbali ya faida hiyo, toka zamani tawi la mti huo linatazamwa kama ishara ya wingi, utukufu na amani. Kwa sababu hiyo lilitolewa kwa miungu na kwa washindi.
Remove ads
Picha
- Mizeituni huko Thassos, Ugiriki.
- Mzeituni wa Bar, Montenegro wenye miaka zaidi ya 2,000
- Zeituni mbichi
- Zeituni mbivu
- Mavuno ya zeituni
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads