Zakayo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Zakayo
Remove ads

Zakayo (kwa Kigiriki Ζακχαῖος, Zakkhaios; kwa Kiebrania זכי, "safi", "asiye na kosa"[1]) alikuwa mtozaushuru tajiri mjini Yeriko aliyepata umaarufu kupitia Injili ya Luka ambayo katika sura ya 19 inasimulia alivyoongoka alipomkaribisha Yesu Kristo nyumbani mwake kwa kumuahidia atawagawia mafukara nusu ya mali yake na kuwarudishia mara nne watu aliowadhulumu kitu.

Thumb
Zakayo alivyochorwa na Niels Larsen Stevns. Yesu anamuita Zakayo ashuke toka juu mtini.
Thumb
Mkuyu wa huko Yeriko leo.
Thumb
"Zakayo akimlaki Yesu",
Kanisa la Mchungaji Mwema, Yeriko.

Kwa kumtafuta mtu kama huyo, aliyetazamwa na Wayahudi kama mpotevu kutokana na kazi yake haramu kwao, Yesu alidhihirisha kwamba alikuja kutafuta waliopotea, wakiwemo matajiri wanaokubali kuachana na uroho ili kujali shida za wengine. Hiyo ni mada muhimu katika Injili hiyo.

Zakayo ni mfano wa kuigwa na matajiri wa leo. Matajiri kwa kawaida yao ni watu wanaojali faida kwa gharama yoyote ile, kwa kupokonya cha maskini ili wafaidike wao. Wanajihalalishia kuwa ni haki yao kuwa matajiri na kuwasahau maskini. Wanachojali ni pesa iingie mifukoni mwao na si vinginevyo.

Inasemekana baadaye alikuwa askofu wa kwanza wa Kaisarea ya Palestina[2]..

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 20 Agosti au 27 Agosti au 20 Aprili au tarehe nyingine[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads