From Wikipedia, the free encyclopedia
Andrea Kim Taegon (Hangul: 김대건 안드레아, Hanja: 金大建; Solmoe, Dangjin, Korea, 1821 – Mto Han, Hanseong, Joseon, sasa Seoul, Korea Kusini, 1846), alikuwa padri wa kwanza wa Kanisa Katoliki mzaliwa wa Korea na ndiye msimamizi wa nchi.
Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri mwaka 1925, halafu tarehe 6 Mei 1984 Papa Yohane Paulo II alimtangaza mtakatifu pamoja na wafiadini wenzake 102 walioshuhudia kwa ushujaa imani ya Kikristo, wakiwemo katekista Paulo Chong Hasang, maaskofu 3, mapadri wengine 7, na walei wengine 91 wa Korea, baadhi wenye ndoa, baadhi wazee, baadhi vijana na hata watoto: wote waliteswa na kuuawa wakikamilisha kwa damu yao mwanzo wa Kanisa nchini [1].
Sikukuu yao wote huadhimishwa kwa pamoja tarehe 20 Septemba[2].
Mwishoni mwa karne ya 18, Ukristo wa Kikatoliki ulianza kuenea taratibu katika rasi ya Korea, nchi ya Kikonfusyo, kwa juhudi na ari za wananchi walei[3].
Mwaka 1836 Korea ilipata wamisionari wa kwanza kutoka nje (wanashirika wa Paris Foreign Missions Society) ambao walilisha na kuthibitisha imani kwa kutangaza Neno la Mungu na kuadhimisha sakramenti [4].
Wazazi wa Andrea waliongokea Ukristo na baadaye baba yake alifia dini hiyo kwa sababu ya kuacha dini yake ya awali.
Baada ya kubatizwa akiwa na umri wa miaka 15, Kim alisoma katika seminari ya Macau (China) na pia Lolomboy, Bocaue, Bulacan, Ufilipino.
Alipewa upadrisho huko Shanghai (1844) akarudi Korea ili kuinjilisha.
Chini ya nasaba ya Joseon, Ukristo ulifutwa, tena waamini walidhulumiwa na kuuawa. Waliobaki walipaswa kushika imani yao kwa siri.
Andrea Kim akawa mmoja kati ya maelfu waliouawa. Mwaka 1846, akiwa na miaka 25, aliteswa na hatimaye kukatwa kichwa karibu na Seoul kwenye Mto Han.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.