Epidemiki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Epidemiki (kutoka Kiingereza epidemic, kiasili ni Kigiriki; pia: epidemia, magonjwa ya mlipuko, mlipuko wa magonjwa) hutokea wakati maambukizi ya ugonjwa fulani yanaenea haraka na kuathiri watu wengi kwa muda mfupi katika eneo fulani.
Kwa mfano, kama maambukizi kutokana na bakteria ya meningococcus (yanayosababisha meninjitisi, yaani ugonjwa wa uti wa mgongo) yanazidi watu 15 kati ya 100,000 katika kipindi cha wiki 2, hali hutazamwa kuwa epidemiki.[1]
Epidemiki inayozidi kuenea na kuathiri nchi mbalimbali, hata Dunia nzima, huitwa pandemia.
Katika kulinda watu dhidi ya kuibuka kwa milipuko mipya, hatua kadhaa mwafaka zimependekezwa na Shirika la Afya Duniani [2]