From Wikipedia, the free encyclopedia
Furukombe, fukombe, kwazi, yowe au tai mlasamaki ni ndege mbuai wa nusufamilia Haliaeetinae katika familia Accipitridae.
Furukombe | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ndege hao ni baina ya tai wakubwa kabisa. Uzito wao unatofautiana kutoka kg 2 (furukombe wa Sanford) mpaka 9 (furukombe wa Steller).
Manyoya yao yana rangi ya kahawia mpaka nyeusi lakini kichwa, mkia, kidari na tumbo ni nyeupe kufuatana na spishi. Furukombe wa Madagaska, wa Sanford na wa Ulaya wana kichwa hudhurungi.
Spishi zote zinatokea karibu na maji ama baridi ama ya bahari. Hula samaki hasa lakini ndege wengine, mizoga na mara kwa mara wanyama wadogo pia.
Hujenga tago lao kwa vijiti juu ya mti au mwamba. Jike hutaga mayai 1-3.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.