From Wikipedia, the free encyclopedia
Visiwa vya Malkia Elizabeth (kwa Kiingereza: Queen Elizabeth Islands, Kifaransa: Îles de la Reine-Élisabeth) ndio kundi la visiwa kaskazini mwa Funguvisiwa la Aktiki ya Kanada. Kiutawala visiwa hivi vimegawanyika baina ya Nunavut na Northwest Territories za Kanada. Visiwa vya Malkia Elizabeth vimefunikwa kabisa kwa barafu ilhali vina takriban asilimia 14 za eneo la barafu na theluji duniani [1] ukiondoa ngao za barafu za Greenland na Antaktiki.
Visiwa hivyo vilipewa jina kwenye mwaka wa 1953, baada ya kutawazwa kwake Elizabeth II kuwa malkia wa Kanada. Kabla ya hapo vilijulikana kama Parry Archipelago kwa zaidi ya miaka 130 tangu kupitiwa na mpelelezi Mwingereza Sir William Parry mnamo 1820.
Kulingana na atlasi ya Kanada kuna visiwa vikubwa 34 na vidogo 2,092 katika funguvisiwa hilo[2]. Kisiwa kikubwa ni Ellesmere Island iliyo na km² 196,235.
Visiwa kwa pamoja vina eneo la kilomita za mraba 419,061[2].
Visiwa hufunika eneo linalofanana na umbo la pembetatu ilhali inapakana na Mlangobahari wa Nares upande wa mashariki, mlangobahari wa Parry upande wa kusini na Bahari ya Aktiki upande wa kaskazini na magharibi.
Visiwa vilivyo vingi havina watu isipokuwa kuna vituo vya utafiti wa tabianchi.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.