Amoni, Zeno na wenzao

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Amoni, Zeno na wenzao Tolomayo, Ingene na Theofilo (walifia dini Aleksandria, Misri, 249 hivi) wakati wa dhuluma ya kaisari Decius.

Habari zao zinapatikana katika Historia ya Kanisa iliyoandikwa na Eusebi wa Kaisarea akiripoti barua ya Dionisi wa Aleksandria kwa Fabio wa Antiokia [1].

Theofilo alikuwa mzee, wengine wanne askari; wakiwa mahakamani wakati Mkristo mwenzao alipokuwa anateswa ili aache imani, walikuwa wanamtia moyo asizidi kuyumba kutokana na maumivu makali. Hapo umati uliwapigia kelele, nao wakajitosa katikati kujitangaza Wakristo wakauawa mara moja [1][2][3].

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama watakatifu wafiadini[4][2][5] .

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 1 Juni[6][7][8].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads