Ana (nabii)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ana (nabii)
Remove ads

Ana (kwa Kiebrania חַנָּה, Hannah, kwa Kigiriki Ἄννα, Anna) alikuwa mwanamke wa karne ya 1 KK katika Israeli.

Thumb
Ana siku ya Yesu kutolewa hekaluni, mchoro wa Giotto, Padova, Italia.

Ni maarufu kama nabii kutokana na habari iliyomo katika Injili ya Luka (2:36-38[1]).

Humo tunaambiwa kwamba alikuwa binti Fanueli, wa kabila la Asheri.

Alipoachwa mjane ujanani baada ya miaka 7 ya ndoa, alihamia hekalu la Yerusalemu akifunga chakula na kusali hadi miaka 84.[2][3][4][5][6][7][8]

Mtoto Yesu alipoletwa hekaluni siku 40 tu baada ya kuzaliwa, Ana alitangaza habari zake kwa waliokuwepo [9].

Tangu kale anaheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo kama mtakatifu nabii.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3[10] au 16 Februari.[11][12]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads