Andrea Avellino

From Wikipedia, the free encyclopedia

Andrea Avellino
Remove ads

Andrea Avellino (Castronuovo di Sant'Andrea, Potenza, 1521Napoli, 10 Novemba 1608), alikuwa padri wa Italia[1] wakati wa Urekebisho wa Kikatoliki akajiunga[2] na aina mpya ya utawa aliyoianzisha Gaetano wa Thiene, maarufu kwa jina la Wateatini, akaieneza zaidi pamoja na kufanya utume.

Thumb
Sanamu yake huko Milano.

Pamoja na kung'aa kwa maisha matakatifu na juhudi kwa wokovu wa wengine, alijifunga kwa nadhiri ngumu ya kupiga hatua kila siku kuelekea ukamilifu wa Kikristo, na hatimaye, akiwa mwingi wa stahili, alifariki altareni.[3].

Alitangazwa na Papa Urban VIII kuwa mwenye heri tarehe 14 Oktoba 1624, halafu Papa Klementi XI alimtangaza mtakatifu tarehe 22 Mei 1712.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads