Aretha mfiadini

From Wikipedia, the free encyclopedia

Aretha mfiadini
Remove ads

Aretha (kwa Kiarabu: الحارث, "al-Haarith") alikuwa kiongozi wa Wakristo Waorthodoksi wa Mashariki wenye asili ya Ethiopia walioishi Najran (leo Ukhdūd nchini Saudia) mwanzoni mwa karne ya 6, wakati wa kaisari Yustino.

Thumb
Mchoro mdogo katika Menologion of Basil II ukionyesha Aretha alivyokatwa kichwa. Wenzake wengi walichomwa moto.

Aliuawa pamoja na wenzake walau 340, kama si 4,000 au 20,000[1] (akiwemo mke wake Ruma na mabinti wao wanne) mwaka 523, wakati wa dhuluma ya mfalme Dhu Nuwas aliyekuwa ameongokea dini ya Uyahudi .[2][3]

Anajulikana kupitia Acta S. Arethae (pia: Martyrium sancti Arethae au Martyrium Arethae)[4][5][6]

Kurani inalaani dhuluma hiyo katika sura LXXXV:4-8.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu mfiadini[7].

Sikukuu yake na ya wenzake huadhimishwa nao tarehe 24 Oktoba[8][9].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads