Waashuru
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Remove ads
Waashuru (kwa Kiaramu ܣܘܪܝܝܐ) ni kabila la Kisemiti la watu wa Mesopotamia kaskazini, ambao leo kwa kiasi kikubwa wanaishi nje ya nchi yao asili (hasa katika Iraq na Syria za leo, pamoja na maeneo madogo ya Uturuki na Iran), hasa Marekani, Ulaya Magharibi na Australia.[1][2][3][4][5][6]
Kwa jumla duniani kote wanakadiriwa kuwa kati ya milioni 2 na 4.25. Wengi wao ni Wakristo (hasa Kanisa Katoliki la Wakaldayo na Kanisa la Waashuru la Mashariki), na kwa sababu hiyo wamedhulumiwa na watawala mbalimbali kwa karibu miaka 2000 mfululizo.[7]
Waashuru wana historia tukufu upande wa ustaarabu na siasa kwa kuwa walirithi na kueneza utamaduni wa Wasumeri na Waakadi ambao ndio wa kwanza duniani katika mambo mengi.
Hasa dola la Ashuru lilistawi kati ya karne ya 24 KK na karne ya 7 KK liliposhindwa na Wakaldayo wa Babuloni (605 KK).
Biblia inazungumzia mara nyingi habari za dola hilo lililokuwa tishio kwa Waisraeli na mataifa mengi ya Mashariki ya Kati kwa muda mrefu.
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads