Kanisa la Wakaldayo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kanisa la Wakaldayo
Remove ads

Kanisa Katoliki la Wakaldayo (kwa Kiaramu ܥܕܬܐ ܟܠܕܝܬܐ ܩܬܘܠܝܩܝܬܐ , ʿītha kaldetha qāthuliqetha) ni mojawapo kati ya Makanisa Katoliki ya Mashariki, likifuata mapokeo ya Mesopotamia na kutumia liturujia ya Mesopotamia[1].

Thumb
Patriarki mstaafu, kardinali Emmanuel III Delly.

Idadi ya waamini leo ni zaidi ya 600,000[2] [3], wengi wao wakiwa wenyeji wa Mesopotamia.

Remove ads

Historia

Kanisa hilo linachanga historia moja na Kanisa la Asiria hasa hadi mwaka 1552, lilipotokea farakano kati yao, huku waliojiita Wakaldayo wakiungana na Kanisa Katoliki kama walivyotangulia kufanya wenzao kadhaa wa Cyprus mwaka 1445[4]

Muundo

Kanisa hilo linaongozwa na Patriarki wa Baghdad, Iraki, kwa sasa Louis Raphaël I Sako (kwa Kisiria: ܠܘܝܣ ܪܘܦܐܝܠ ܩܕܡܝܐ ܣܟܘ) aliyezaliwa tarehe 4 Julai 1948 na anayeishi Baghdad.[5]

Chini yake kuna majimbo katika nchi hiyo (250,000 waamini), katika nchi nyingine za Mashariki ya Kati (Iran, Siria, Uturuki, Lebanon na Misri) na kwenye mtawanyiko uliotokana na waamini kuhama kwa sababu ya hali ngumu hasa ya vita na dhuluma: Marekani, Kanada, Australia na New Zealand n.k.

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads