Baali
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Baali (maana yake mmiliki au Bwana katika lugha za Kisemiti za Kaskazini zilizotumika huko Mashariki ya Kati ya kale) ni jina lililokuja kutumika kwa ajili ya miungu, hasa kwa mungu wa dhoruba na wa uzazi, Hadad.

Biblia ya Kiebrania inalitumia mara 90 kuhusiana na miungu mbalimbali ya makabila jirani na Waisraeli waliosadiki Mungu mmoja tu na kuona hiyo mingine kuwa miungu bandia tu. Biblia inaeleza ibada za makuhani wa Baali [1], na hasa shindano lililoitishwa na nabii Eliya juu ya mlima Karmeli ili kuwaonyesha Waisraeli yupi ni Mungu wa kweli kati ya YHWH na Baali dhidi ya juhudi za malkia Jezebeli za kueneza kati yao dini ya taifa lake (Tiro) [2].
Matumizi hayo yaliingia katika Ukristo[3] na Uislamu[4], pengine kwa umbo la dharau Beelzebub, kuhusu pepo.
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Marejeo mengine
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads