Bethlehemu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Betlehemu (kwa Kiarabu "بيت لحم", Beit Lahm) maana yake ni "Nyumba ya mkate" (kutoka Kiebrania בית לחם, ambapo "בית" = nyumba na "לחם" = "mkate") ni mji wa Palestina, maarufu hasa kama mahali alipozaliwa Yesu Kristo kadiri ya Injili ya Mathayo[1] na Luka[2].


Kadiri ya Mathayo, ndivyo ulivyotimia utabiri wa kitabu cha Mika 5:1.
Mapokeo yanataja mahali hapo katika Kanisa la Kuzaliwa lililojengwa mnamo mwaka 330 kwa amri ya Kaizari Konstantino.
Bethlehemu iko kilometa 10 hivi kusini kwa Yerusalemu, mita 765 juu ya usawa wa bahari. Kwa sasa ina wakazi zaidi ya 25,000 ambao wanategemea hasa utalii.
Remove ads
Historia
Inakadiriwa kuwa Bethlehemu ilianzishwa miaka 1,400 KK.
Kadiri ya Biblia, Bethlehemu ndio mji asili wa Daudi, mfalme wa pili wa Israeli na babu wa Yesu katika mfululizo wa vizazi vingi.
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads