Bethlehemu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Bethlehemu
Remove ads

Betlehemu (kwa Kiarabu "بيت لحم", Beit Lahm) maana yake ni "Nyumba ya mkate" (kutoka Kiebrania בית לחם, ambapo "בית" = nyumba na "לחם" = "mkate") ni mji wa Palestina, maarufu hasa kama mahali alipozaliwa Yesu Kristo kadiri ya Injili ya Mathayo[1] na Luka[2].

Thumb
Mandhari ya Bethlehemu.
Thumb
Kanisa la Kuzaliwa kwa Yesu mjini Bethlehemu

Kadiri ya Mathayo, ndivyo ulivyotimia utabiri wa kitabu cha Mika 5:1.

Mapokeo yanataja mahali hapo katika Kanisa la Kuzaliwa lililojengwa mnamo mwaka 330 kwa amri ya Kaizari Konstantino.

Bethlehemu iko kilometa 10 hivi kusini kwa Yerusalemu, mita 765 juu ya usawa wa bahari. Kwa sasa ina wakazi zaidi ya 25,000 ambao wanategemea hasa utalii.

Remove ads

Historia

Inakadiriwa kuwa Bethlehemu ilianzishwa miaka 1,400 KK.

Kadiri ya Biblia, Bethlehemu ndio mji asili wa Daudi, mfalme wa pili wa Israeli na babu wa Yesu katika mfululizo wa vizazi vingi.

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads